Maalim Seif awataka wajumbe wa CUF kuwa makini

Monday, 11 March 20130 comments


        sefu

Ushiriki wa wajumbe katika vikao vya chama kikamilifu ni muhimu kwa maendeleo ya kuimarisha  na kuboresha  uhai wa chama.
Wito huo umetolewa leo na katibu mkuu wa chama cha wananchi cuf  ambae pia  ni  Makamo wa kwanza wa Rais wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar katika mkutano mkuu wa wilaya uliofanyika katika ukumbi wa jamat-hani Zanzibar.
Katika mkutano huo Maalim Seif amewataka wajumbe hasa hasa wa ngazi za chini kuwa makini na kutilia umuhimu vikao vya chama kwani  vikao ndio vinavyotoa maamuzi yaliyo sahihi sambamba na kuonesha uhai wa chama.
Aidha amewata wajumbe kuhakikisha wanawafuatilia wanachama kulipia ada, pamoja na kushiriki katika harakati  za kisiasa ikiwa ni pamoja na kuimarisha  mikusanyiko ya pamoja kupeana  taarifa mbali mbali kuhusu zinazoendelea  Nchini.
Pia Maalim Seif  amefahamisha kuwa harakati za uchaguzi wa ndani ya chama zinakaribia  hivyo amewataka wanachama kujitokeza kugombania nafasi hizo pamoja na kuwakemea baadhi ya viongozi wa cuf ambao wanalengo la kuwagawa wanachama kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Aidha ametowa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika ushiriki wa kujiandikisha katika vitambulisho vya taifa sambamba na kuhakikisha wanapata kadi zao za ukaazi.
Amewataka wananchi kutoa ushirikiano  kwa jeshi la polisi kuhakikisha wanawapata wale ambao wanasababisha  matokeo ya hujma nchini sambamba na serikali kutoa taarifa ilioyo bayana kwa wananchi.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Zanzibar News - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger