Chama cha Wananchi CUF kimewataka wanachama wake huko kisiwani Pemba kuendeleza umoja na mshikamo walionao ili waweze kuifanya Zanzibar kuwa na mamlaka kamili.
Hayo yamesemwa na Tamim
Omari Tamim ambae alikuwa miongoni mwa wanachaama ADC kwa sasa amejiunga na CUF wakati alipokuwa akiwahutubia Wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika leo huko viwanja vya Masota Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Tamim amewataka Wananchama wa CUF kisiwani humo wasije
wakajaribu kabisa kumfuata Hamad Rashia kwani
kufanya hivo kutakuwa ni sawa na watu waliojisaliti wenyewe.
'Watu walikufa kwa ajili ya chama hiki leo uhame kwa
hadaa ya kibwetere huyu Hamad Rashid musijaribu ndugu zangu, sisi tumemjua dhamira
yake ndio maana tuka toka' alisema Tamim
Nae Makamo Mwenyekiti wa
Chama cha Wananchi CUF Tifa Machano Khamis Ali amewataka wafuasi wa chama hicho
kuhakikisha wanakuwa wa mwanzo kujitokeza katika kuandikisha Vitambulisho vya
Taifa muda ukifika.
Kwani kufanya hivo kutaweza
kukifanya Chama hicho kushinda katika uchaguzi unaofata “kama
tunavojua CCM wananjama nyingi wanaweza
kusema mtu asiekuwa na kitambulisho asipige
kura katika uchaguzi unaofata’’alisema Machano.
Chama hicho bado kinaendelea
na mikutano yake ya uimarishaji wa Chama ambapo kwa siku ya kesho kitafanya
mkutano wa hadhara huko katika kijiji cha Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa
Kaskazini Pemba mnamo majira ya saa nane mchan.
Post a Comment